Friday, October 1, 2010

WAANDISHI WA HABARI WAWILI WASHAMBULIWA

*      Hii ni dalili mbaya kwa kazi za kuihabarisha jamii na taaluma kwa ujumla
*      Hofu yatanda kwa waandishi wengine kanda ya magharibi ambako zipo issues nyingi za maendeleo

Katika kile kinachodhaniwa kuwa ni kuzima harakati za wanahabari na vyombo vya habari kusaidia jamii kujua masuala mabali mbali ya maendeleo na hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi, waandishi wa habari wawili wanaofanya kazi katika jiji la Mwanza nchini Tanzania hivi karibuni wameshambuliwa huku mmoja akiswekwa ndani kwa agizo la kiongozi mmoaj wa serikali.

Dhahama hilo linaloenda kinyume cha katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya kumi na nane inayotoa uhuru wa kutoa au kupata habari, limemkumba mwakilishi wa idhaa ya kishwahili ya BBC London Bw. Erick David Nampesya, pamoja na Mwandishi wa magazeti ya Mwananchi Communication Bw. Fredrick Katulanda naye ameonja joto la jiwe mara tatu mfululizo, ambapo anataja kuwa alishambuliwa na watu wasio julikana nyumbani kwake na kasha kutoweka bila kupora chochote zaidi ya suluba dhidi ya mwili wake.

Akiongea na Kigoma Leo kwa njia ya simu, Erick David anaeleza kuwa alishambuliwa na mgambo wa jiji la mwanza na kisha kusweka rupango kwa agizo la mkurugenzi wa jiji la mwanza Bw. Wilson

Bw. Nampesya ameeleza kuwa kilichotokea ni mkurugenzi wa jiji kuchukizwa na habari iliyotangazwa na BBC kuhusu shule nyingi za msingi katika jiji la Mwanza kutokuwa na vyoo hali inayohatarisha afya za watoto na kushuka pia kwa kiwango cha elimu katika jiji hilo.

Na kana kwamba haitoshi mwandishi Fredrick Katulanda hivi karibuni yeye aliambulia kichapo pale alipokuwa wakifuatilia mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu hapa nchini.

Bw. Katulanda amedai kufuatiliwa na watu asio wajua na kwamba siku moja akiwa nyumbani alivamiwa na kupigwa na watu wapatao wanne na kisha kutoweka bila kujulikana.

Amebainisha kuwa katika tukio la pili alizuiliwa kuendelea na msafara wa kampeni za mgombea Urais wa chama cha mapinduzi DR. Jakaya Kikwete katika mikkoa ya kanda ya ziwa, ingawa ametaja kuwa kitendo hicho hakikutokana na amri ya Kikwete bali wapambe wake.

Katika tukio jingine, Bw. Katulanda alipigwa na kufukuzwa eneo la mkutano wa kampeni za chama cha mapinduzi mkoani Mwanza baada ya kiongozi mmoja wa chama hicho kuwaamuru vijana wa CCM maarufu kwa jina la Green Guard kuwafukuza waandishi wa habari katika mkutano wao na pale walipotaka kujua sababu za kufukuzwa, ndipo walipotandika na kulazimika kukimbilia polisi

Matukio haya ya kupigwa au kuzuiliwa kuandika habari kunakowatokea wanahabari Tanzania ni matokeo ya uwajibikaji mdogo wa viongozi ambao wanaposhindwa kutimiza wajibu wao kwa wananchi hutafuta mbinu za kuzuia maovu yao yasiangazwe.