Saturday, September 18, 2010

AJALI ZA BARABARANI ZINAVYOUA NGUVU KAZI MKOANI KIGOMA

Jumla ya watu hamsini na sita wakiwemo abiria na madreva wa magari wamepoteza maisha katika ajali za barabarani katika kipindi cha January 2009 hadi june 2010 katika mkoa wa Kigoma nchini Tanzania na kupelekea taifa kupoteza nguvu kazi na kushuka kwa uchumi wa kaya za marehemu.

Kwa mujibu wa kitengo cha usalama barabarani cha jeshi la polisi Tanzania ajali zilizosababisha vifo vya watu hao zilitokana na ubovu wa miundombinu ya usafiri ikiwemo barabara pamoja na uzembe au uchakavu wa magari yanayotumiwa na ab iria kwa ajili ya safari.

Mkuu wa usalama barabarani mkoa wa Kigoma ASP William Mkonda ameeleza kuwa katika kipindi cha mwaka 2009 jumla ya ajali zilizotokea zilikuwa 379 wakati akatika kipindi cha January hadi june 2010 tayari ajali 380 zimetokea

Bw. Mkonda ameeleza kuwa abiria waliopoteza maisha ni 42 wakati amdeva walifariki tisa hadi june mwaka huu na kwamba uaharibifu mkubwa wa mali umetokea ikiwa ni pamoja na kusababisha majeruhi kufikia idadi ya watu 90.

Mkuu huyo wa usalama barabarani mkoa wa Kigoma amefafanua kuwa licha ya uzembe wa abiria, madereva na wamiliki wa magari, ajali nyingine hutokana na waenda kwa miguu na watumiaji wengine wa vyombo vya moto hususani pikipiki pamoja na baiskeli.

Jumla ya waendesha pikipiki 7 na waendesha baiskeli 6 wameripotiwa kufariki dunia katika matukio mbalimbali ya ajali za barabarani mkoani Kigoma, wakati waliojeruhiwa wakitajwa kuongezeka siku hadi siku kutokana na ajali za pikipiki.

Aidha ukosefu wa elimu ya usalama barabarani ni moja ya changamoto zinazoukabiri mkoa wa kigoma katika suala la matumizi ya barabara na vyombo vya usafiri.

Kutokana na changamoto hizo jeshi la polisi limeelezea azima yake ya kuanzisha mkakati wa ukaguzi madhubuti wa magari kabla ya safari pamoja na utoaji wa elimu kwa abiria na madereva, na kwa wanafunzi katika shule za msingi na sekondari ili kupunguza ajali za barabarani.

No comments:

Post a Comment