Wednesday, September 22, 2010

TAKUKURU YAPIGA MKWARA WAANDISHI WA HABARI KIGOMA, TABORA, SINGIDA NA DODOMA

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Tanzania imetoa tahadhari kwa waandishi wa habari watakaokiuka kanuni za maadili na sheria ya kuzuia Rushwa na sheria ya uchaguzi kuwa haitasita kuwachukulia hatua za kisheria kama wakosaji wengine.

Tahadhari hiyo imetolewa na mkuu wa taasisi hiyo mkoa wa Dodoma Bi. Eunice Mmari wakati akifungua mkutano wa siku moja wa waandishi wa habari kutoka miko aya Kigoma, tabora, Singida na Dodoma iliyofanyika katika hoteli ya Dodoma Hotel jumanne wiki hii.

Bi. Mmari alieleza kuwa taifa linawatarajia sana wanahabari katika kuelimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali ya kutimiza wajibu kwa jamii na viongozi wa vyama vya siasa, wagombea na wapiga kura wakati wa uchaguzi na hivyo isingekuwa vema wana habari nao kuhusika katika kukiuka sheria.

Alisisitiza kuwa baadhi ya waandishi wa habari wamekuwa wakilaumiwa kwa kuomba fedha kutoka kwa wadau ili waandike habari zao jambo ambalo ni kinyume cha sheria ya gharama za uchaguzi namba sita na sheria ya Rushwa namba 11 ya taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania.

Bi. Mmari alisisitiza kuwa vyombo vya habari ni mmhimili mkubwa sana na tarajio la taifa katika kujenga maadili katika jamii na miongoni mwa watumishi wa umma, hivyo ni vema wakazingatia kanuni za maadil wakati wa kuandika na kuripoti habari za uchaguzi mkuu wa wabunge, madiwani na rais mwaka huu wa 2010.

Kwa upande wao wanahabari walioshiriki mafunzo hayo, wametaja changamoto m,balimbali zinazowakabiri mikoani katika kuandika habari za uchaguzi na kutaja kuwa vyombo vya habari na wamiliki wake havitoi kipaumbele kwao tofauti na wanavyofanya kwa waandishi walioko Dar es salaam.

Wanahabari hao wamelalamikia pia vitendo vya baadhi ya wahariri kuegemea vyama au wagombea na kupelekea habari zinazoandikwa kutoka mikoani dhidi ya wagombea au vyama Fulani kutoandika magazetini au kutangazwa katika radio na Runinga.

Aidha wameonya kuwepo kwa wamiliki wa habari ambao ni wadau wa kisiasa na wadhamini wa vyama ambao huwataka wahariri wao kutoandika habari za mgombea au chama fulanai na kushirikiza vyombo vyao kuvitangaza vyama vingine zaidi kuliko vyama vya wapinzani wao.

Mafunzo ya kanuni za maadili ya uandishi wa habari za uchaguzi mwaka huu yalidhaminishwa na mpango wa elimuya uchaguzi chini ya shirika la mapango wa maendeleo duniani UNDP na kuhudhuriwa na wanahabari zaidi ya arobaini kutoka kanda ya kati na magharibi.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment