Tuesday, September 7, 2010

HOFU YA POLIO MKOANI KIGOMA

Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na shirika la afya duniani, limebaini kuwepo kwa uwezekano wa kuibuka kwa maambukizi ya ugonjwa wa polio katika mipaka ya Tanzania na jamhuri ya Kidemohrasia ya Kongo DRC.



Akiongea na Channel afrika kwa njia ya simu, Mganga mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dr. Valentino Bangi amebainisha kuwa kutokana na mawasialiano ya ujirani mwema pamoja na ukaguzi wa taarifa mbalimbali za kiafya katika mipaka hiyo, serikali ya Tanzania imepata taarifa kuwa nchini DRC kuna maambukizi ya Polio.



Dr. Bangii amebainisha kuwa kutokana na taarifa hizo, wizara ya afya kwa kushirikiana na WHO wameandaa mkakati kabambe wa kutoa chanjo kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano katika wilaya ya Kigoma inayopakana na DRC mwambao wa ziwa Tanganyika.



Amesema kiasi cha dozi laki moja cha chanjo ya polio kimekwisha wasili mkoani Kigoma na zoezi la uchanjaji lilianza jumamosi August 21, 2010.



Kwa upande wake idara ya afya katika bandari ya Kigoma inayotoa huduma za usafiri na usafirisdhaji wa mizigo kwenda DRC, Burundi na Zambia, imeelezwa kuwa maafisa wa afya wamejiweka tayari kukagua na kutoa chanjo kwa abiria watoto wanaoingia nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment